Numbers 24:1-6
1 aBasi Balaamu alipoona imempendeza Bwana kubariki Israeli, hakuendelea tena kutafuta uchawi kama nyakati nyingine, bali aligeuza uso wake kuelekea nyikani. 2 bBalaamu alipotazama nje na kuona Israeli amepiga kambi kabila kwa kabila, Roho wa Mungu akawa juu yake, 3 cnaye akatoa ujumbe wake: “Ujumbe wa Balaamu mwana wa Beori,ujumbe wake yeye ambaye jicho lake linaona vizuri;
4 dujumbe wake yeye ambaye husikia maneno ya Mungu,
ambaye huona maono kutoka kwa Mwenyezi, ▼
▼ Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania (pia 24:16).
ambaye huanguka kifudifudi, na ambaye macho yake yamefunguka:
5 f“Tazama jinsi yalivyo mazuri mahema yako, ee Yakobo,
maskani yako, ee Israeli!
6 g“Kama mabonde, yanaenea,
kama bustani kando ya mto,
kama miti ya udi iliyopandwa na Bwana,
kama mierezi kando ya maji.
Copyright information for
SwhKC